Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 31, 2016

Mwana wa Besigye awania urais Oxford

Mwana wa kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza
Besigye ni miongoni mwa wanafunzi waliojitokeza
kuwania urais katika chama cha mijadala chuo cha
Oxford.
Anselm Besigye ametengeneza video fupi ya kuwaomba
wanafunzi wenzake wampigie kura.
Anasimulia mambo ambayo amefanyia chama hicho na
uzoefu wake katika mijadala.
Mwisho wa video mamake Anselam Winnie Besigye,
anaonekana na kusema “huna budi kushinda uchaguzi
huu, nimekusaidia sana!”.
Babake Anslem, Dkt Kizza Besigye, amewania urais
mara nne dhidi ya kiongozi wa muda mrefu wa Uganda
Yoweri Museveni bila mafanikio.
Anazuiliwa kwake nyumbani na maafisa wa usalama
tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu tarehe 20 Februari.