Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, March 23, 2016

Afisa mwingine wa jeshi auawa Burundi

Afisa mwengine wa ngazi ya juu katika jeshi la Burundi
ameuwawa usiku wa jana katika hali ya kutatanisha
katikati mwa jiji la Bujumbura.
Meja Didier Mihimpundu ameuawa saa chache baada ya
kuuawa kwa kamanda wa kambi moja muhimu mjini
Bujumbura Kanali Darius Ikurakure akiwa kwenye makao
makuu ya jeshi mjini Bujumbura .
Kamanda wa kambi ya Bujumbura Kanali Darius
Ikurakure ameuawa
Meja Didier Muhimpundu aliuawa karibu saa mbili ya
usiku .
Polisi wanasema alipokea simu na kuondoka ndani ya
baa moja mjini Bujumbura kabla ya kufyatuliwaa risasi.
Hadi sasa waliomuuwa afisa huyo aliyekuwa msimamizi
wa idara ya afya ya jeshi , hawajafahamika kwa mujibu
wa naibu msemaji wa polisi Moise Nkurunziza.
'' Meja Muhimupundu alipigiwa simu na mtu akiwa
katika baa, halafu alipotoka kutaka kukutana na mtu
huyo, wakampiga risasi, na akafariki papo hapo,''
''Uchunguzi umeanzishwa kujua vema watu hao
waliofanya ukatili huo , na hivo wafikishwe mbele ya
vyombo vya sheria kuadhibiwa. alisema Nkurunziza.
Saa moja kabla ya Meja Muhimpundu kuuwawa,
kulisikika milio ya risasi Kaskazini mwa jiji katika mtaa
wa Carama .
Wakaazi sehemu hiyo wanathibitisha polisi mmoja
aliuwawa katika ufyatulianaji huo wa risasi.
Hata hivo polisi imekanusha taarifa hizo na kutaja kuwa
alitekwa.
'' Polisi huyo alitekwa na watu waliokuwa katika gari la
watu binafsi, ambao walikuwa wamevalia sare za
kijesh.''
''Taarifa za kuuliwa kwake si sahihi hazina ukweli
maana haijaonekana maiti yake'' alisema msemaji wa
polisi Nkurunziza.
Awali jana mchana aliuwawa Kamanda wa kambi moja
muhimu ya kijeshi hapa nchini Luteni Kanali Darius
Ikurakure akiwa ndani ya makao makuu ya jeshi hapa
mjini Bujumbura.
Mauaji hayo ya mfululizo yameanza kutafsiriwa kama
ulipizanaji kisasi katika jeshi lenye mchanganyiko wa
makabila na kutishia uwiano wa vikosi vya ulinzi.
Msemaji wa Jeshi Clement Cimana .ameonya kuhusu hali
hiyo'' Makao Makuu ya jeshi yanalaani vikati ukatili
wowote wa aina hii,uongozi wa jeshi unawatolea wito
wanajeshi popote walipo kubaki wanashikamana na
kuwaepuka watu wanaojaribu kuwagawanya kwa lengo la
kusambaratisha jeshi la Burundi.''
Katika kipindi cha miezi minane , maafisa wakuu jeshini
wasiopungua watano wameuawa katika jiji la Bujumbura,
lakini mauaji ya sasa yameibuka baada ya siku kadhaa
za utulivu nchini

Related Posts:

  • Paris yakumbwa na Mafuriko Mto Seine ulioko mjini Paris, Ufaransa, umejaa na kufikia kima cha juu zaidi kuwahi kutokea kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita. Maji yamefurika hadi kwenye barabara na kulazimisha makavazi kadhaa na maeneo ya makaburi kufungwa… Read More
  • UM kupeleka misaada zaidi nchini Syria Maafisa wa kibalozi jijini New York wanasema kuwa hiyo kesho Umoja wa Mataifa utaomba rasmi Serikali ya Syria kuruhusu kudondosha vyakula na madawa katika maeneo wanakoishi wananchi walio katika hatari ya kufa kutokana n… Read More
  • Marufuku wapenzi wa jinsia moja kuasili watoto DRCBunge la Seneti la Jamhuri ya kidemkrasia ya Congo limepiga marufuku wapenzi wa jinsia moja kuwaasili watoto kutoka nchi hiyo. Serikali imekuwa mstaari wa mbele ikijaribu kupeleleza hatma ya watoto waliohamishwa nje ya nchi… Read More
  • Suluhu ya Israel na Palestina hatarini Matumaini ya kupatikana kwa suluhu ya mataifa mawili katika mgogoro wa Israel-Palestina yako hatarini,waziri wa maswala ya kigeni nchini Ufaransa Jean-Marc Ayrault ameonya. ''Lazima hatua za haraka zichukuliwe'',alisema k… Read More
  • Mohammed Ali Afariki Aliyeluwa bondia wa kwanza maarufu mweney asili ya Kiafrika, Mohammed Ali, wa Marekani amefariki leo asubuhi akiwa na umri wa miaka 74. Kulingana na msemaji wa familia yake, bingwa huyo wa zamani wa uzani wa juu, anayeju… Read More