Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, March 23, 2016

Mshukiwa wa mashambulio ya Brussels ‘atambuliwa’

Mshukiwa aliyekuwa akisakwa sana kuhusiana na
mashambulio ya Brussels ametambuliwa na maafisa wa
usalama, vyombo vya habari Ubelgiji vimeripoti.
Baadhi ya vyombo vya habari limetaja jina lake kuwa
Najim Laachraoui.
Wadadisi wanasema Laachraoui anaaminika kuwa
mtaalamu wa kuunda mabomu.
Alionekana kwenye picha ya kamera za usalama uwanja
wa ndege akiwa pamoja na washukiwa wawili ambao
inadaiwa walijilipua wakati uwanja wa ndege wa
Zaventem.
Alikuwa tayari anatafutwa na polisi kuhusiana na
mashambulio ya Paris mwaka jana.
Ripoti za kukamatwa kwake bado hazijathibitishwa na
maafisa wa usalama.
Taarifa za awali zilikuwa zimewatambua washukiwa
walioonekana naye kwenye uwanja wa ndege kuwa ndugu
wawili, Brahim na Khalid El Bakraoui.
Watu 34 walifariki na zaidi ya 250 kujeruhiwa kwenye
mashambulio mawili yaliyotokea katika uwanja huo wa
ndege wa Zaventem na kituo cha treni cha Maelbeek.
Kundi linalojiita Islamic State limedai kutekeleza
mashambulio hayo.
Bendera zinapepea nusu mlingoti nchini Ubelgiji. Taifa
hilo limetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

Related Posts:

  • Wekeza katika maarifa "Until your brain sweat, you won't experience swiftness" Katika kitabu cha Hosea 4:6 imeandikwa “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa…” Inawezekana umesikia mara nyingi sehemu hii; swali ambalo nataka tujiulize kwa… Read More
  • Kufikiri vizuri kumenifikisha hapa  Makala hii ni miongoni mwa makala za hayati Munga Tehenan, zilizowahi kutoka katika Gazeti la Jitambue. (Gazeti hilo limesimama kuchapishwa kutokana na sababu za kiufundi)Nimeamua kuirejea makala hii kwa sababu ina… Read More
  • msimdharau mshindani wako Don’t underestimate your rival   Ikiwa mhitimu wa chuo kikuu ataambiwa ajiandae kwa mtihahi wa darasa la kwanza, nadhani maandalizi pekee atakayofanya ni kwenda kwenye huo mtihani ambao unaonekana ni wa chini sana ukil… Read More
  • Nguvu ya kufikiri Chanya   Kila mmoja wetu ana namna yake ya kufikiri na hizi namna tofauti za kufikiri ndizo ambazo zinatutofautisha binadamu. Ni tofauti hizi pia ambazo zinatufanya tuwe na tofauti katika mafanikio maishani mwetu. Wale ambao… Read More
  • wanawake wanawapenda wanaume wasio waoga   Katika utafiti wa hivi karibuni, watafiti wamegundua kwamba, wanawake wanawapenda wanaume wasio waoga na mashujaa kuliko wale waoga. Ushujaa wa wanaume ni kigezo kikubwa kwa wanawake kuwapenda marafiki wa kiume wa mu… Read More