Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 17, 2016

Wafuasi 89 wa Boko Haram wahukumiwa kifo Cameroon

Wanachama 89 wa kundi la Kiislamu la Boko Haram
nchini Nigeria wamehukumiwa kifo nchini Cameroon
baada ya kupatikana na makosa kujihusisha na ugaidi.
Wanachama hao wamehukumiwa na mahakama ya kijeshi
kwa mchango wao katika mashambulio kadha eneo la
kaskazini mwa Cameroon linalopakana na Nigeria, kwa
mujibu wa idhaa ya BBC Hausa.
Eneo hilo limekuwa likishambuliwa mara kwa mara na
wanamgambo wa Boko Haram.
Waliohukumiwa ni sehemu ya wanachama 850
wanaozuiliwa nchini Cameroon kwa kudaiwa kuhusika na
mashambulio ya kundi hilo la Kiislamu.
Hii ni mara ya kwanza kwa watu kuhukumiwa kifo chini
ya sheria mpya za kukabiliana na ugaidi zilizopitishwa
mwaka 2014.
Sheria hiyo hupendekeza kifo kwa wanaopatikana na
makosa ya ugaidi.
Watu 22 walihukumiwa kifo mwaka 2013.

Related Posts:

  • 10 Reasons You Need to Road Trip with Your Family! So here are 10 Great Reasons to Road Trip with your family!  1) It’s time to disconnect! Leave the office behind. Power down your computer and that smart phone. Give this time to your spouse and kids, and allow old-f… Read More
  • MAGAZETI YA LEO MEI 2 Read More
  • Ajipiga risasi akitafuta 'Selfie ya mwaka'Polisi India wamesema kuwa kijana mmoja amejipiga risasi kichwani kimakosa,akitafuta mbinu ya kujipiga picha ya ''selfie'' ya kipekee akiwa na bastola ya babake. Kijana huyo mwenye umri wa miaka 15 anaendelea kupokea matibabu… Read More
  • Reaching Your Destiny Reaching your destiny requires taking each of the following steps in the corresponding order: 1. Thoughts – Everything that you see in the world--except for what grows naturally--begins as a thought. Our light fixtur… Read More
  • Ukame: Burkina Faso kutoa maji kwa mgao Burkina Fao itaanza ugavi wa maji katika mji mkuu Ouagadougou, kutokana na ukosefu mkubwa wa maji. Waziri mmoja alisema kuwa serikali imeamua kufunga maji kwenda wilaya tofauti za mji baada ya kila saa 12. Wiki chache ziliz… Read More