Kiongozi wa jimbo la Galmudug, katikati mwa Somalia
amesema wanajeshi wa jimbo hilo wamewaua zaidi ya
wapiganaji 100 wa al-Shabab kwenye mapigano
yaliyodumu siku nne.
Wapiganaji hao wa Kiislamu walikuwa wameingia jimbo
hilo wakitoroka mapigano mengine kaskazini katika jimbo
la Puntalnd.
Rais wa jimbo hilo Abdikarin Hussen Gulled ameambia
BBC kwamba wapiganaji 100 waliuawa na wengine
wengi kukamatwa.
Habari hizo hazijathibitishwa na taasisi nyingine.
Wapiganaji 30 wa al-Shabab wauawa Puntland
Wapiganaji wa al-Shabab walikuwa wamekabiliana na
wanajeshi wa jimbo la Puntland linalopakana na
Galmudug mapema wiki iliyopita.
Wamekuwa wakihamia maeneo ya kaskazini baada ya
kukabiliwa na wanajeshi wa Somalia wakisaidiwa na
wanajeshi wa nchi za Umoja wa Afrika (Amisom)
maeneo ya kusini na kati mwa Somalia.
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
8 hours ago