Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 17, 2016

AU kutuma waangalizi wa uchaguzi Zanzibar

Tume ya Umoja wa Afrika imetangaza kwamba
itawatuma waangalizi wa uchaguzi wa marudio visiwani
Zanzibar ambao utafanyika Jumapili.
Mwenyekiti wa tume hiyo Dkt Nkosazana Dlamini Zuma
ameidhinishwa kutumwa kwa wataalamu sita wa kufuatilia
uchaguzi huo wa tarehe 20 Machi.
Vyama sita vya upinzani, kikiwemo Chama cha
Wananchi (CUF) vimetangaza kwamba vitasusia
uchaguzi huo.
Uchaguzi huo unatokana na kufutwa kwa matokeo ya
uchaguzi wa urais na wawakilishi uliofanyika tarehe 25
Oktoba mwaka jana.
Chama cha CUF kilipinga hatua ya kufutwa kwa
matokeo hayo .
Mgombea wake wa urais, Maalim Seif Sharif Hamad,
alijitangaza mshindi wa uchaguzi huo wa mwaka jana.
CUF kususia marudio ya uchaguzi Zanzibar
Sababu 8 za kufutwa kwa uchaguzi Zanzibar
Juhudi za kutumia mazungumzo kutafutia ufumbuzi mzozo
wa kisiasa uliotokana na kufutwa kwa matokeo hayo
hazikufua dafu.
Kupitia taarifa, AU imesema: “Kuambatana na wajibu
wake, Tume ya Umoja wa Ulaya itatuma ujumbe wa
wataalamu Zanzibar kuhakikisha kwamba uchaguzi wa
marudio ni wa amani, wa kuaminika na unatimiza
viwango vya AU vya uchaguzi wa kidemokrasia.”
Ujumbe huo utakuwa visiwani Zanzibar kati ya tarehe
17 na 25 Machi.

Related Posts:

  • Simu zinaweza kufichua siri kuhusu maisha yako Chembechembe zinazopatikana kwenye simu za mikononi zinaweza kuashiria kiwango cha afya na maisha ya mmiliki, ikiwemo matibabu na aina ya chakula anachopendelea. Wanasayansi kutoka California waligundua chembechembe za ka… Read More
  • What is 'Hyperinflation'What is 'Hyperinflation' Hyperinflation is extremely rapid or out of control inflation. There is no precise numerical indication of hyperinflation. Hyperinflation is a situation where the price increases are so out of control… Read More
  • Korea kaskazini: tupo tayari kwa vita kamili. Korea Kaskazini imeionya Marekani kutoanzisha vitendo vya uchokozi katika eneo la Korea ikisema kuwa iko tayari kulipiza kisasi kupitia mshambulio ya kinyuklia. Taifa hilo limesema hivyo wakati ambapo kiongozi wa Korea Kaskaz… Read More
  • Tanzania yaanza kujenga reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro Rais wa Tanzania John Magufuli leo hii ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi mkubwa wa reli ya kisasa ya Standard Gauge ambayo hapo baadae itaunganisha nchi za Rwanda na Burundi pia. Lakini katika … Read More
  • Familia ya dinosaria yapatikana TanzaniaMojawapo ya jamii wa awali wa dinosaria alikuwa na maumbile yanayofananishwa na mamba, matokeo ya utafiti Tanzania yanaonyesha. Wataalam wa masuala ya uhifadhi wa mabaki ya wanyama wamejiuliza familia ya dinosari wa kitambo w… Read More