Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 31, 2016

Daraja laporomoka na kuwaua 10 India

Takriban watu 10 wameuawa na wengine kadhaa
kujeruhiwa baada ya daraja moja la juu lililokuwa
likijengwa kuporomoka kwenye mji wa mashariki mwa
India wa Kolkata
Ripoti zingine zinasema kuwa karibu watu 150 huenda
wamekwama chini ya vifusi vya daraja hilo lililo eneo
lenye shughuli nyingi.
Miradi ya ujenzi nchini India mara nyingi imekumbwa
na matatizo ya kiusalama na huporomoka mara kwa
mara.
Wataalamu wanasema kuwa, huwa kuna ukosefu wa
ukaguzi wa miradi na matumizi ya vifaa duni katika
ujenzi.