Recent Posts

PropellerAds

Monday, March 14, 2016

Putin aagiza jeshi lake kuondoka Syria

Rais wa Urusi Vladimir Putin ametoa amri kwa
wanajeshi walioko Syria kurejea nyumbani mara moja
kwa sababu tayari wametekeleza asilimia kubwa ya
malengo yao.
Akizungumza katika ikulu ya Kremlin Putin, alisema
''Tayari tumeshakamilisha asilimia kubwa ya madhumuni
yetu nchini Syria kwa hivyo kuanzia jumanne (kesho)
ningependa asilimia kubwa ya jeshi letu kurejea
nyumbani.'' alisema bwana Putin.
Tangazo hilo lake limewaacha wachanganuzi wengi
wamepigwa na mshangao kwani hakukuwa na dalili
zozote za kuwepo kwa tukio kama hilo.
Aidha Putin ametangaza hilo katika siku ambayo
mazungumzo ya amani yameanza upya mjini Geneva
Uswisi.
Urusi ni mshirika wa karibu sana wa rais wa Syria
Bashar al-Assad.
Ikulu ya Kremlin inasema kuwa rais Bashar al-Assad
alifahamishwa kuhusu hatua hiyo.
Itakumbukwa kuwa kuingia kwa majeshi ya Urusi katika
vita vya Syria vilibadili kabisa taswira ya vita hivyo.
Kwa wakati huo waasi walionekana kuwa walikuwa
wanaelekea kuishinda nguvu jeshi la Syria kinyume na
hali ilivyo sasa ambapo majeshi watiifu kwa rais Assad
wameanza hata kuteka maeneo yaliyokuwa chini ya
waasi.
Rais Putin hata hivyo amesema kuwa kambi ya kijeshi
ya Hmeimim na bandari ya Tartus itasalia chini ya jeshi
la Urusi.
Huku akisisitiza kuwa zitalindwa ''kwa hewa ardhini na
hata baharini''

Related Posts:

  • Trump amteua jaji wa mahakama kuu Neil Gorsuch Rais Donald Trump amemteua Neil Gorsuch kujaza nafasi katika mahakama kuu kwa mwaka mmoja . Bw Gorsuch mwenye umri wa miaka 49 ni jaji katika mahakama ya rufaa mjini Denver. Jaji huyo hatarajiwi kutoa hukumu juu ya utoaji m… Read More
  • Mama atakiwa ''kuthibitisha anatoa maziwa'' uwanja wa ndege Mwanamke mmoja amewasilisha malalamishi yake kwa maafisa wa polisi wa Ujerumani akidai kuwa aliambiwa atoe maziwa katika eneo la usalama la uwanja wa ndege ili kuthibitisha kuwa ananyonysha mtoto. Gayathiri Bose aliambi… Read More
  • Your Weakness Is Not Meaningless God has given you so many limitations because he loves you. If you’re like most people, you don’t feel loved by your limitations. You feel confined, stunted, trapped, and exposed by them. You feel discouraged by how we… Read More
  • AU kujiondoa katika mahakama ya ICC Umoja wa Afrika umeunga mkono mpango wa kujiondoa kwa pamoja katika mahakama ya ICC ambayo mataifa mengi ya Afrika yanahisi inawalenga viongozi wa bara la Afrika pekee. Uamuzi huo uliochukuliwa katika kikao cha faragha ha… Read More
  • Kenya: Majirani zetu walitusaliti AUWaziri wa maswala ya nchi za kigeni Kenya Amina Mohammed Mgombea wa wadhfa wa mwenyekiti kutoka Kenya katika tume ya Umoja wa Afrika AU Amina Mohammed ametaja usaliti mio… Read More