Wakuu katika serikali ya Jamhuri ya Congo
wameamrisha kampuni mbili kuu za simu, kufunga
mawasiliano yote ya simu, wakati wa uchaguzi wa urais
hapo kesho.
Wizara ya mashauri ya ndani ya nchi ilisema imefunga
mawasiliano kwa sababu za usalama.
Mgombea wa upinzani, John Marie Michel Mokoko,
alisema amepokea amri ya kwenda polisi, na alisema
hiyo ni hatua ya kumzuia yeye katika kugombea
uchaguzi.
Wagombea wanane wanampinga Rais Denis Sassou
Nguesso.
Katiba ilibadilishwa mwaka jana, kumruhusu agombee
tena uongozi.
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
8 hours ago