Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, March 22, 2016

Watu 31 wauawa katika mashambulio Brussels

Watu 31 wamefariki baada ya mashambulio kutekelezwa
katika uwanja wa ndege wa Zaventem na kituo cha
treni cha Maelbeek mjini Brussels.
Waziri wa afya wa Ubelgiji amesema watu 11 walifariki
na wengine 81 kujeruhiwa baada ya milipuko miwili
kutokea uwanja wa ndege wa Zaventem, nje kidogo ya
mji wa Brussels.
Meya wa Brussels amesema watu 20 walifariki
Maelbeek.
Kundi linalojiita Islamic State limedai kutekeleza
mashambulio hayo
Waziri Mkuu wa Ufaransa Francois Hollande amelaani
mashambulio hayo mjini Brussels na kusema ni kama
mashambulio yaliyolenga bara lote la Ulaya.
Waziri Mkuu wa Ubelgiji Charles Michel amesema hatua
zaidi zimechukuliwa kuimarisha usalama mpakani.
Kwa Picha: Mashambulio ya Brussels
Mshukiwa wa Paris alitaka kujilipua
Mchezaji wa DR Congo anusurika Brussels
Milipuko hiyo imetokea siku nne tu baada ya kukamatwa
kwa mshukiwa mkuu wa mashambulio ya Paris ya
mwaka jana ambayo yalisababisha vifo vya watu 130.
Abdeslam alikamatwa Ijumaa katika mtaa mmoja wa
Brussels.
Uwanja wa ndege wa Zaventem unapatikana kilomita 11
kaskazini mashariki mwa Brussels na ulihudumia abiria
zaidi ya 23 milioni mwaka jana.

Related Posts:

  • China targets African support in Western institutions In October 1971, when Mao Zedong’s People’s Republic of China (PRC) tussled with Taiwan for membership of the United Nations, the former won in no small part thanks to its African allies. Twenty-six African countries voted f… Read More
  • A Privileged PositionYou are my friends if you do what I command (John 15:14, NIV). What could be a greater privilege than to have Jesus call us His friend? If I told you that the president of the Tanzania was my friend, you would probably sni… Read More
  • When money grows on trees Alan Paul, the 62-year-old chairman of EFK Group, originally realised the nut’s potential when he worked as a consultant researching biofuels. In 2012 he founded a backyard operation based on this natural product “lite… Read More
  • HERE ARE THE 100 BEST EDUCATION INFOGRAPHICS “Education is the most powerful weapon which you can use to change the world.”–Nelson Mandela With the world around us ever-changing, education is now more important than ever. Beginning as early as prehistory as a means to… Read More
  • Al shabaab waua polisi 5 Mandera Kenya Maafisa 5 wa polisi wa Kenya wameuawa mapema leo mjini Mandera katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al shabab kutoka Somalia. Kamishna wa jimbo hilo la kaskazini mashariki mwa Kenya b… Read More