Chama cha Democtratic Alliance nchini Afrika Kusini
kumeanzisha kampeni ya kumuondoa rais Jacob Zuma
madarakani baada ya mahakama ya kikatiba kutoa
uamuzi kuwa alikiuka katiba.
Mahakama ilipata kuwa bwana Zuma alikataa kutii agizo
kutoka kwa ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu mwaka
2014 la kamtaka alipe pesa zilizotumika kuifanyia
ukarabati nyumba yake ya kibinafsi.
Vyama viwili vya upinzani viliwasilisha kesi hiyo
mahakamani ili kumlazimu rais Jacob Zuma kuzingatia
matokeo ya uchunguzi yaliofanywa na mkaguzi wa hesabu
za serikali, kwamba alihusika na mabadiliko yaliofanyiwa
nyumba yake ya Nkandla.
Mamilioni ya madola yalitumika katika kile kilitajwa na
serikali kuwa uimarishaji wa usalama. Marekebisho hayo
yalishirikisha ukumbi,kidimbwi cha kuogelea na zizi la
ngombe
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
9 hours ago