Recent Posts

PropellerAds

Monday, March 28, 2016

Sharif aahidi kuangamiza magaidi Pakistan

Waziri Mkuu wa Pakistan Nawaz Sharif ametoa wito
kwa kuwepo ushirikiano zaidi kati ya idara za usalama
nchini humo ili kukabiliana na ugaidi.
Amesema hayo siku moja baada ya watu zaidi ya 70
kuuawa kwenye shambulio la bomu katika mji wa
Lahore. Kiongozi huyo ameahidi kuwaangamiza magaidi
hao.
Bw Sharif, aliyekutana na viongozi wa idara za
usalama, amesema taifa hilo litaimarisha juhudi za
kukabiliana na ugaidi.
Watu kadha wamekamatwa na silaha kupatikana kwenye
operesheni iliyofanywa na vikosi vya usalama, jeshi
limesema.
Kundi la Jamaat-ul-Ahrar lililotokana na kundi la
Taliban limekiri kutekeleza shambulio hilo.
Watu 300 walijeruhiwa na maafisa wa serikali
wamesema idadi ya waliofariki inatarajiwa kupanda.
Eneo hilo lilikuwa na watu wengi kuliko kawaida, kwani
Wakristo walikuwa wamekusanyika katika bustani
kusherehekea Pasaka.
Facebook yaomba radhi kuhusu Pakistan
Taliban wakiri kuhusika shambulio Pakistan
Hata hivyo, wengi wa waliofariki walikuwa Waislamu.
Mmoja wa waliofariki, mvulana Mkristo Sahil Pervez,
alizikwa Jumatatu.
Bw Sharif alitembelea majeruhi hospitalini.
Baadaye katika mkutano na maafisa wa usalama,
alisema ni jambo la umuhimu mkubwa kuwashinda
magaidi.
“Azma yetu kama taifa na serikali inaendelea kuwa
thabiti na adui huyu mwenye uoga anajaribu kushambulia
watu wasio na silaha,” amesema.
Aliapa kuwa serikali yake itawaangamiza magaidi hao
walioua “wanangu”.
Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis kwa
upande wake ametoa wito kwa serikali ya Pakistan
kulinda makundi ya kidini ya wachache nchini humo.