Polisi nchini Mali wanasema watu wawili wamekamatwa
kaskazini mwa nchi, kwa kuhusika na shambulio
lilofanywa mwezi huu na Al Qaeda, katika eneo la
watalii nchini Ivory Coast.
Mmoja wao anasemekana kuwa ndiye aliyepanga usafiri
wa washambuliaji.
Mwenzake anatuhumiwa kuwa mshauri mkuu kiongozi wa
njama hiyo.
Wanaume wote wawili ni raia wa Mali.
Watu 19 waliuwawa pale wanaume waliokuwa
wamejihami kwa silaha kali kuingia kwa nguvu katika
eneo la pwani, la Grand Bassam, karibu na mji mkuu,
wa Ivory Coast, Abidjan.
Waliwapiga risasi waliokuwa wakikoga ufukweni, kabla ya
kuivamia hoteli.
Habari kubwa Magazetini Kenya leo May 4, 2024
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania May 4, 2024,nakukaribisha
kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini
keny...
13 hours ago