Waziri wa zamani wa Rwanda Jacques Bihozagara
amefariki katika gereza moja nchini Burundi miezi minne
baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kufanya ujasusi.
Rwanda imesema marehemu Jacques alikuwa ameshikiliwa
kinyume cha sheria.
Balozi wa Rwanda nchini Ubelgiji ameandika na kusema
kifo cha Jacques ni "mauaji".
Wafungwa katika gereza alipokuwa ameshikiliwa
wanasema alionekana akiwa katika hali nzuri na kwamba
alifariki dakika chache baada ya kuchukuliwa kutoka
gereza kupelekwa hospitali baada ya kuugua.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukiishutumu Rwanda kwa
kujaribu kuipindua serikali ya Rais wa Burundi Pierre
Nkurunziza, madai ambayo Rwanda imekuwa
ikiyakanusha.
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
9 hours ago