Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, March 30, 2016

Ajali ya ndege yawaua watu 7 Canada

Watu saba wamefariki baada ya ndege moja ya kibinafsi
kuanguka katika kisiwa cha mashariki ya pwani ya
Quebec.
Mamlaka imesema kuwa ndege hiyo ilianguka ilipokuwa
ikikaribia uwanja wa ndege wa Madeleine huku kukiwa
na upepo mkali pamoja na barafu.
Jean Lapierre,aliyekuwa waziri wa uchukuzi nchini
Canada pamoja na watu wa familia yake walikuwa
miongoni mwa waathiriwa.
Bwana Lapierre mwenye umri wa miaka 59,alifanya kazi
kama mchanganuzi wa CTV pamoja na vyombo vyengine
vya habari.
Mojawapo ya vituo hivyo TVA kilisema mkewe Lapierre
,nduguze wawili na dadaake mmoja walifariki katika
ajali hiyo.