Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, March 30, 2016

Ajali ya ndege yawaua watu 7 Canada

Watu saba wamefariki baada ya ndege moja ya kibinafsi
kuanguka katika kisiwa cha mashariki ya pwani ya
Quebec.
Mamlaka imesema kuwa ndege hiyo ilianguka ilipokuwa
ikikaribia uwanja wa ndege wa Madeleine huku kukiwa
na upepo mkali pamoja na barafu.
Jean Lapierre,aliyekuwa waziri wa uchukuzi nchini
Canada pamoja na watu wa familia yake walikuwa
miongoni mwa waathiriwa.
Bwana Lapierre mwenye umri wa miaka 59,alifanya kazi
kama mchanganuzi wa CTV pamoja na vyombo vyengine
vya habari.
Mojawapo ya vituo hivyo TVA kilisema mkewe Lapierre
,nduguze wawili na dadaake mmoja walifariki katika
ajali hiyo.

Related Posts:

  • MAGAZETI YA LEO JUNE 3. Read More
  • Dawa zilimuua Prince:Madaktari Uchunguzi wa kidaktari kutoka jimbo la Minnesota nchini Marekani umebaini kuwa mwanamuziki Prince alikufa kutokana na kuzidisha kiwango cha dawa. Kwa mujibu wa madaktari waliofanya uchunguzi huo wa kifo cha mwanamuziki… Read More
  • Miili ya wahamiaji yapatikana:Libya Taarifa kutoka Libya zinasema kuwa miili ya watu wanaodaiwa kuwa ni wahamiaji, imepatikana ikiwa imetapakaa katika mwambao wa bahari karibu na mji wa Zuwara. Baadhi ya taarifa zinasema zaidi ya miili 85 imeonekana ikiwa… Read More
  • India yaanzisha huduma ya kusambaza maji matakatifu Serikali ya India imesema kuwa inajiandaa kuzindua huduma za kusambaza maji matakatifu na chakula kupitia ujumbe. Waziri anayesimamia huduma ya kutuma ujumbe ya posta Ravi Shankar Prasad amesema kuwa maji kutoka kwa maeneo… Read More
  • Wataka sheria ya talaka kufutwa India Wanaume na wanawake 50,000 wamesaini azimio la kushinikiza serikali ya India kufutilia mbali sheria ya kutumia neno Talaq, mara tatu kwa misingi ya kuvunja ndoa. Kwa sasa wanaume Waislamu wanaweza kuwataliki wake zao kwa… Read More