Recent Posts

PropellerAds

Friday, March 25, 2016

Akamatwa kwa kuipelelezea Korea Kusini

Raia wa Marekani aliyekamatwa nchini Korea Kaskazini
amesema kuwa aliiba siri za kijeshi za Korea kaskazini
ili kuisaidia Korea Kusini katika taarifa na waandishi wa
habari ilioandaliwa na Pyongyang.
Kim Dong Chul mwenye umri wa miaka 62 alikiri
kufanya hivyo siku ya ijumaa,akiomba msamaha kwa
kupeleleza.
Bwana Kim awali aliwaambia waandishi kwamba yeye ni
raia wa Marekani aliyezaliwa nchini Korea Kusini na
kwamba alikamatwa mwezi Oktoba kwa kufanya
upelelezi.
Bwana Kim amesema kwamba alikutakana na maafisa wa
upelelezi kutoka Korea Kusini mwaka 2011 ili kuifanyia
uchunguzi,kulingana na shirika la habari la KCNA
kutoka nchini Korea Kaskazini.
Alikamatwa wakati alipokuwa akichukua habari za
kijasusi za kijeshi na zile za kinyuklia kutoka kwa mtu
ambaye hakutajwa.