Kumekuwa na mapigano kati ya wanajeshi wa kenya na
wanamgambo wa al-Shabaab katika eneo la Lower Juba
nchini Somalia.
Kuna ripoti za kukanganya kuhusu maafa.
Wanajeshi wa Kenya wanasema kuwa walivisiwa lakini
wakafanikiwa kuwaua wanamgabo 21 licha ya wao
kupoteza wanajeshi wawili.
Al-Shabab nao wanadai kuwa waliwaua wanajeshi 20
wa Kenya wakawakamata wawili na kuharibu magari yao
sita.
Mapigano hayo yalitokea kwenye barabara inayoelekea
mji wa Afmadow ambapo wanajeshi wa kenya waliwaua
wanamgambo 19 wa al-Shabab siku ya Jumatano.
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
8 hours ago