Recent Posts

PropellerAds

Saturday, March 26, 2016

Wagombea warushiana matusi Marekani

Wagombeaji wawili wa Urais wa chama cha Republican
nchini Marekani wamegombana vikali na kurushiana
matusi juu ya wake zao.
Seneta wa Texas, Ted Cruz, amemlaumu mpinzani
wake, mfanyabiashara Donald Trump kwa kuzusha uvumi
kuwa yeye alikuwa mzinifu na kumdanganya mkewe,
Heidi.
Bwana Cruz alisema uvumi huo ni takataka na akasema
kuwa anaelewa kuwa uvumi ulianzishwa na Bwana Trump
ambaye alisema hastahili kuwa Rais.
Bwana Trump alisisitza kuwa hakuhusika vyo vyote na
uvumi huo.
Mapema juma hili, Bwana Trump alimlaumu Seneta Cruz
kwa kuweka picha za mkewe, Melania, akiwa uchi
kwenye mtandao ili kumharibia sifa.