Wagombeaji wawili wa Urais wa chama cha Republican
nchini Marekani wamegombana vikali na kurushiana
matusi juu ya wake zao.
Seneta wa Texas, Ted Cruz, amemlaumu mpinzani
wake, mfanyabiashara Donald Trump kwa kuzusha uvumi
kuwa yeye alikuwa mzinifu na kumdanganya mkewe,
Heidi.
Bwana Cruz alisema uvumi huo ni takataka na akasema
kuwa anaelewa kuwa uvumi ulianzishwa na Bwana Trump
ambaye alisema hastahili kuwa Rais.
Bwana Trump alisisitza kuwa hakuhusika vyo vyote na
uvumi huo.
Mapema juma hili, Bwana Trump alimlaumu Seneta Cruz
kwa kuweka picha za mkewe, Melania, akiwa uchi
kwenye mtandao ili kumharibia sifa.
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania March 3, 2025,nakukaribisha
kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini
ke...
5 weeks ago