Wagombeaji wawili wa Urais wa chama cha Republican
nchini Marekani wamegombana vikali na kurushiana
matusi juu ya wake zao.
Seneta wa Texas, Ted Cruz, amemlaumu mpinzani
wake, mfanyabiashara Donald Trump kwa kuzusha uvumi
kuwa yeye alikuwa mzinifu na kumdanganya mkewe,
Heidi.
Bwana Cruz alisema uvumi huo ni takataka na akasema
kuwa anaelewa kuwa uvumi ulianzishwa na Bwana Trump
ambaye alisema hastahili kuwa Rais.
Bwana Trump alisisitza kuwa hakuhusika vyo vyote na
uvumi huo.
Mapema juma hili, Bwana Trump alimlaumu Seneta Cruz
kwa kuweka picha za mkewe, Melania, akiwa uchi
kwenye mtandao ili kumharibia sifa.
Wanafunzi Kapeta,Kiwira warithishwa ari ya utunzaji mazingira
-
Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), kwa kushirikiana na Shirika la
Utangazaji la Tanzania (TBC), wameendesha zoezi la upandaji miti katika
Shule ya msi...
8 hours ago