Recent Posts

PropellerAds

Monday, March 28, 2016

Aliyesaidia El Chapo kulangua pesa anaswa

Maafisa wa usalama nchini Mexico wamemkamata
mwanamume wanayesema alisaidia kulangua pesa kwa
niaba ya mlanguzi wa mihadarati Joaquin Guzman,
aliyejulikana sana kama "El Chapo" au "Shorty".
Juan Manuel Alvarez Inzunza, kwa jina la utani "King
Midas", alikamatwa akiwa likizoni katika jimbo la
Oaxaca, kusini mwa nchi hiyo.
Guzman, kiongozi wa zamani wa genge la Sinaloa, kwa
sasa anasubiri kuhamishiwa Marekani akajibu mashtaka.
Alikamatwa Januari baada yake kutoroka jela mwaka
jana.
Bw Inzunza anashukiwa kulangua takriban $300m-
$400m kwa niaba ya genge la Sinaloa kupitia mtandao
wa kampuni na vituo vya kubadilisha pesa za kigeni.
Mahakama ya dola mjini Washington iliomba Inzunza
akamatwe na huenda akapelekwa Marekani kujibu
mashtaka.
Guzman mwenyewe anatakiwa Marekani akajibu mashtaka
ya ulanguzi wa mihadarati California, na mauaji Texas.