Wataalamu nchini Uingereza wanasema wamevumbua
teknolojia ya kusoma midomo ya watu ambayo inaweza
kubaini wanasema nini bila kusikia wanachosema.
Teknolojia hiyo inaweza kusaidia sana kufahamu watu
wanaonaswa kwenye kamera za siri za CCTV wanasema
nini.
Wataalamu hao katika chuo kikuu cha East Anglia
wanasema teknolojia hiyo inaweza kutumiwa kukabiliana
na uhalifu na ugaidi.
Lakini pia inaweza kutumiwa na wanahabari wanaofuatilia
habari za wasanii na watu mashuhuri.
Watu ambao wamekuwa wakitumiwa kujaribu kusoma
midomo ya watu wamekuwa wakitatizika sana
kutofautisha sauti kama vile P na B.
Lakini wanasayansi hao wanasema teknolojia hiyo mpya
inaweza kutofautisha sauti hizo.
Wataalamu hao wanasema pia kwamba teknolojia hiyo
mpya itasaidia sana katika mifumo ya kukusanya habari
kwa kutumia kompyuta.
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania March 3, 2025,nakukaribisha
kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini
ke...
5 weeks ago