Recent Posts

PropellerAds

Friday, March 18, 2016

Simba aingia jijini Nairobi na kujeruhi mzee

Simba aliyetoka katika mbuga ya taifa ya wanyama ya
Nairobi amemshambulia mzee mmoja jijini humo mapema
asubuhi.
Simba huyo alitoka mbugani na kuonekana karibu na
eneo la City Cabanas, katika ya Mombasa Road.
Afisa wa mawasiliano wa Shirika la Huduma kwa
Wanyamapori (KWS) Bw Paul Udoto ameambia BBC
kwamba mzee aliyejeruhiwa ni wa umri wa miaka 63
na amepewa matibabu ya dharura katika uwanja wa
ndege wa Jomo Kenyatta kisha akakimbizwa hospitalini
kwa matibabu kamili.
Hata hivyo, Bw Udoto amesema mzee huyo hayuko
hatarini.
Kwa mujibu wa afisa huyo, simba huyo huenda alikerwa
na kelele za magari yaliyokuwa yakipita.
Vikosi vitatu vya maafisa wa KWS vilitumwa kumdhibiti
na kwa mujibu wa Bw Udoto, simba huyo anaelekezwa
ndani kwenye mbuga.
Maafisa wanaendelea kushika doria kubaini iwapo kuna
simba wengine walitoka mbugani.
Visa vya simba kutoka mbugani vimekuwa vikiripotiwa
siku za karibuni. Mwezi mmoja uliopita, simba wanne
waliingia maeneo ya makazi eneo la Langata.
Wiki mbili zilizopita, simba wawili walidaiwa kuonekana
karibu na barabara ya Ngong.

Related Posts:

  • Trump Aamuru Ndege za Kivita Zianze Kuruka Kuelekea Korea Kaskazini Ndege hatari na mpya zilizotengenezewa kwa teknolojia ya hali ya juu za F-35 Stealth Fighter Jets tayari zimeruka kutoka jimbo la Utah lililopo magharibi mwa nchi ya Marekani na kutua UK tayari kabisa kwa training ya mwisho … Read More
  • The Effects Of Negative Emotions On Our Health Humans experience an array of emotions, anything from happiness, to sadness to extreme joy and depression. Each one of these emotions creates a different feeling within the body. After all, our body releases different che… Read More
  • Familia ya dinosaria yapatikana TanzaniaMojawapo ya jamii wa awali wa dinosaria alikuwa na maumbile yanayofananishwa na mamba, matokeo ya utafiti Tanzania yanaonyesha. Wataalam wa masuala ya uhifadhi wa mabaki ya wanyama wamejiuliza familia ya dinosari wa kitambo w… Read More
  • Korea kaskazini: tupo tayari kwa vita kamili. Korea Kaskazini imeionya Marekani kutoanzisha vitendo vya uchokozi katika eneo la Korea ikisema kuwa iko tayari kulipiza kisasi kupitia mshambulio ya kinyuklia. Taifa hilo limesema hivyo wakati ambapo kiongozi wa Korea Kaskaz… Read More
  • What is 'Hyperinflation'What is 'Hyperinflation' Hyperinflation is extremely rapid or out of control inflation. There is no precise numerical indication of hyperinflation. Hyperinflation is a situation where the price increases are so out of control… Read More