Recent Posts

PropellerAds

Saturday, March 19, 2016

Mlipuko wawauwa watu 4 Uturuki

Gavana wa Istanbul, Uturuki, anasema watu wanne
wameuwawa katika mripuko wa bomu kufuatia shambulio
la kujitolea mhanga katikati ya mji.
Watu wengine kama 20 wamejeruhiwa.
Picha za televisheni zimeonesha magari ya kubeba
wagonjwa, yakielekea eneo la mashambulio, ambalo sasa
limetengwa na polisi.
Jumapili iliyopita, shambulio jengine lilifanywa katika mji
mkuu wa Uturuki, Ankara, na kuuwa watu 37.
Chama cha waopiganaji wa KiKurd, TAK, kilisema
kilihusika na shambulio hilo.