Recent Posts

PropellerAds

Thursday, March 31, 2016

Trump ayumbayumba kuhusu utoaji mimba

Mgombea urais wa chama cha Republican nchini
Marekani Donald Trump amebadili msimamo wake muda
mfupi baada ya kusema wanawake wanaotoa mimba
wanafaa kuadhibiwa, utoaji mimba ukiharamishwa.
Alikuwa ametoa tamko lake katika hafla iliyopeperushwa
moja kwa moja na kituo cha runinga cha MSNBC.
Hatua hiyo ilimfanya kushutumiwa vikali.
Lakini muda muda mfupi baadaye, alibadili msimamo
wake na kusema ni wahudumu wa afya wanaosaidia
wanawake kutoa mimba pekee wanaofaa kuadhibiwa.
Lakini hata baada ya kusema hivyo, alijitetea na
kuongeza kuwa: “Msimamo wangu haujabadilika.”
Mgombea huyo anayeongoza katika chama cha
Republican anaunga mkono kupigwa marufuku kwa utoaji
mimba, lakini kwa kutegemea hali.
Utoaji mimba umekuwa halali nchini Marekani tangu
1973 kufuatia uamuzi wa kihistoria wa Mahakama ya
Juu nchini humo.
Trump aahidi kuvunja mkataba wa nyuklia
Trump akemewa kwa matamshi kuhusu Waislamu
Mambo 20 makuu anayoamini Donald Trump
Ni kupitia Mahakama Kuu pekee au marekebisho ya
katiba ambapo uamuzi huo katika kesi ya Roe v Wade
unaweza kubatilishwa na uavyaji mimba kuharamishwa.
Bw Trump, ambaye wakati mmoja alikuwa mfuasi wa
chama cha Democratic, ameshutumiwa awali kwa kutetea
haki za wanawake kutoa mimba.
Msimamo rasmi wa chama cha Republican ni kwamba
utoaji mimba unafaa kuwa haramu.
Wanasiasawahafidhina na wanaharakati wanaochukulia
utoaji mimba kuwa sawa na mauaji, hata hivyo, mara
nyingi hukwepa kuwekea lawama wanawake wanaotoa
mimba na badala yake kuwalaumu wanaowasaidia
wanawake kutoa mimba.
Lengo kuu la hili huwa kuvutia wananchi ambao kimsingi
hawawezi wakafurahia kuwaona wanawake wengi
walioshika mimba kimakosa wakifungwa jela kwa kutoa
mimba.
Viongozi wa chama cha Republican wameeleza wasiwasi
wao kuhusu kuidhinishwa kwa Bw Trump kuwa mgombea
wa chama hicho katika uchaguzi mkuu Novemba, hasa
kwa sababu kura za maoni zinaonesha hapendwi sana
na wapiga kura wa kike.
Bw Trump ameshutumiwa kwa kuwadhalilisha wanawake
wakiwemo aliyekuwa mgombea urais Carly Fiorina na
mtangazaji wa runinga Megyn Kelly.
Meneja wake, Corey Lewandowski, alikamatwa Jumanne
akituhumiwa kumshambulia mwanahabari wa kike.
Bw Trump amemtetea Bw Lewandowski akisema
hakutenda kosa lolote.

Related Posts:

  • Yawning at Majesty Let’s say you were given this assignment: construct a book that will remain relevant for millennia and radically influence the greatest civilizations in the history of the world. How would you do it? Would you think that … Read More
  • Malalamiko sita (6) ya Malaika Kati ya viumbe vyote ambavyo Mungu ameviumba  hakuna kiumbe hata kimoja chenye thamani kumshinda Mwanadamu. Mwanzo1:1 Hapo mwazo  Mungu aliziumba mbingu  na nchi, Mwanzo 1:26 Mungu akasema, na tumfanye&nb… Read More
  • We Believe in the Holy Spirit We believe in the Holy Spirit. That reality is more than meets the eye. That God is alive and at work in our world, and in our lives. That an unseen Person prompts, protects, and provides for those who are Christ’s. That a… Read More
  • What Does It Mean to Seek the Lord? Seeking the Lord means seeking his presence. “Presence” is a common translation of the Hebrew word “face.” Literally, we are to seek his “face.” But this is the Hebraic way of having access to God. To be befor… Read More
  • Everything for God’s Glory I have a kind of person in my mind, and I do so because of a recent conversation at my church. And this is such a typical conversation. There’s nothing extraordinary about it. Any pastor in the room has had it. Most of you… Read More