Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, March 16, 2016

Korea Kaskazini yatishia kuishambulia Marekani

Korea Kaskazini imetishia kutekeleza mashambulio ya
nyuklia dhidi ya Korea Kusini na Marekani iwapo nchi
hizo mbili zitaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi.
Mazoezi hayo, ambayo hufanyika kila mwaka, mwaka
huu yatashirikisha wanajeshi 300,000.
Serikali ya Korea Kaskazini imetoa taarifa ya ikitishia
kutekeleza “shambulio la nyuklia kwa ajili ya haki”.
Ni kawaida kwa Pyongyang kutoa vitisho vya aina hiyo
na wataalamu wanatilia shaka uwezo wa Korea
Kaskazini kuwa na makombora ya nyuklia.
Hisia hupanda kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini
na Marekani kila mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi
yanapofanyika.
Pyongyang hutazama mazoezi hayo kama mazoezi ya
kujiandaa kuivamia.
Korea Kaskazini kuweka tayari silaha za nyuklia
Mhubiri wa Canada afungwa maisha Korea Kaskazini
Korea Kaskazini yatangaza kamanda mpya wa jeshi
Mwaka uliopita, Korea Kaskazini ilitishia kugeuza
Washington kuwa “bahari ya moto”.
Wizara ya ulinzi ya Korea Kusini imeionya Pyongyang
dhidi ya “hatua za haraka zisizo za busara ambazo
zinaweza zikailetea maangamizi”.
Mazoezi ya mwaka huu, yanayoshirikisha wanajeshi
300,000 wa Korea Kusini na 15,000 wa Marekani,
ndiyo makubwa zaidi kuwahi kufanyika.
Yanaandaliwa siku chache tu baada ya Umoja wa
Mataifa kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Korea
Kaskazini kutokana na hatua yake ya kufanyia majaribio
bomu la nyuklia na kufyatua makombora.
Korea Kaskazini ilijibu vikwazo hivyo kwa kutangaza
itaweka tayari silaha zake za nyuklia na pia ikavyatua
makombora ya masafa mafupi baharini.

Related Posts:

  • Orodha ya Mataifa fisadi zaidi Afrika MasharikiBaada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kunaswa na kamera akiidunisha Nigeria kuwa mafisadi wakuu kote duniani BBC imeamua kuangazia kwa umakini ikiwa matamshi hayo ni ya kweli. Je Nigeria imeorodheshwa katika nafasi … Read More
  • Besigye akamatwa kwa 'kujiapisha' UgandaTaharuki imetanda nchini Uganda baada ya kiongozi wa upinzani Dr Kizza Besigye, ''kujiapishwa kama rais'' siku moja tu kabla ya kuapishwa rasmi kwa rais Yoweri Museveni . Haijulikani ni vipi Dr Kiiza Besigye alikwepa kizuizi … Read More
  • Walimu walipwa vifaranga badala ya mshahara Uzbekistan Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa. Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan wamekua wakitia vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na u… Read More
  • Rais Yoweri Museveni aapishwaYoweri Museveni leo ametawazwa rasmi kuwa Rais mpya wa Uganda kwa muhula wa tano mfululizo.Tayari Rais Museveni amekwisha tawala miaka 30. Kutawazwa kwake leo, ambako kunashuhudiwa na viongozi wa mataifa 14 kutoka Afrika na w… Read More
  • Everton yamfuta kazi kocha wake Klabu ya Everton imempiga kalamu mkufunzi wake Roberto Martinez baada ya kuifunza klabu hiyo kwa miaka mitatu. Kilabu hiyo ya Martinez ilio katika nafasi ya 12 katika jedwali li ligi ya Uingereza ilishindwa 3-1 na mabingw… Read More