Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, May 25, 2016

Hukumu kesi ya shambulio la Al-Shabab Uganda

Mahakama mjini Kampala leo inatarajiwa kutoa
hukumu katika kesi ambapo wanaume 13
wameshtakiwa kuhusiana na mashambulio ya mabomu
yaliyotekelezwa na al-Shabaab mwaka 2010.
Watu zaidi ya 70 walifariki kwenye mashambulio hayo
yaliyotekelezwa watu wakitazama fainali ya Kombe la
Dunia la mwaka 2010.
Kesi hiyo imechukua miaka sita.
Baadhi ya washtakiwa walikuwa wameambia
mahakama kwamba waliteswa na maafisa wa ujasusi
wa kanda, Marekani na Uingereza.
Lakini mahakama ya kikatiba nchini Uganda ilifutilia
mbali madai hayo.
Washtakiwa 13
Washukiwa ni 13 kutoka Uganda, Kenya na Tanzania.
Saba ni Waganda, 5 Waenya na mmoja anatoka
Tanzania.
Wao ni: Bw Habib Suleiman Njoroge, Isa Ahmed Luyima
Abubaker Betamatory na Dkt Ismail Kalule.
Wengine ni Suleiman Hijar Nyamandondo, Hassan
Haruna Luyima, Hussein Hassan Agade, Bw Idris
Magondu, Mohamed hamid Suleiman na Yahya
Suleiman Mbuthia.
Kutokea kwa shambulio
Shambulio lilifanyika 11 Julai, 2010 na vituo viwili
vilishambuliwa Ethiopian Village Restaurant, Kabalagala
na Kyadondo Rugby Club, Nakawa watu waliopokuwa
wamekusanyika kutazama fainali ya Kombe la Dunia
iliyokuwa ikichezewa Afrika Kusini.
Idadi ya wahanga
Watu 74 walifariki katika shambulio hilo na wengine 70
kujeruhiwa. Takriban watu 60 waliouawa ni wa kutoka
Uganda. Wengine waliofariki dunia ni kutoka mataifa ya
Ethiopia, Eritrea, India na Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo pamoja na mmoja kutoka Ireland na Marekani.
Kuendeshwa kwa kesi
Kesi ilianza miaka mitano baadaye baada ya
kucheleweshwa na hatua ya washukiwa kupinga
kupelekwa kwao nchini Uganda na kudai kuteswa na
vikosi vya usalama.
Lakini Oktoba 2014 mahakama ya kikatiba ilitupilia
mbali kesi yao na hivyo kesi kuanza.
Wanashtakiwa makosa ya: ugaidi, mauaji na kuwa
wanachama wa kundi la kigaidi.
Jaji wa mahakama kuu aliyesikiliza kesi hiyo ni jaji
Alfonso Owiny Dollo.
Mwendesha mashtaka kuuawa
Wakati mmoja muongoza mashtaka aliuawa na watu
wasiojulikana waliokuwa na bunduki.

Related Posts:

  • what is truthTruth, like knowledge, is surprisingly difficult to define. We seem to rely on it almost every moment of every day and it's very "close" to us. Yet it's difficult to define because as soon as you think you have it pinned d… Read More
  • Never Argue about Religion by Rick Pimentel The Table Talk series focuses on everyday issues that we discuss with one another and have philosophical significance. The previous Table Talk articles dealt with common sense and minding our own busine… Read More
  • Forcing the Will to Believe By Richard Pimentel "Should a civilised, tolerant society get into so personal a matter as the religious conviction of its citizens? After all, what is so perverse about conversion? If you exercise your fundamental… Read More
  • Beautiful, Isn't It? by Richard Pimentel No doubt, Monty Python’s Monty Python and the Holy Grail is one of the funniest movies of all time. The entire cast of Monty Python is certainly one of the funniest comedy casts ever assembled. Who can… Read More
  • How (Other) People Change Walking with Loved Ones Through Five Stages Read More