Recent Posts

PropellerAds

Thursday, May 26, 2016

Mugabe asema kuwa haondoki madarakani

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kuwa
yeye sio Mmarekani wala Muingereza wakati
akiwahutubia karibu watu 50,000, wafuasi wake
kwenye mkutano uliofanyika kwenye mji mkuu Harare
kwa heshima yake.
Mugabe mwenye umri wa miaka 92 amekana
uwezekano wowote wa kuondoka madaraklani na
kuwashambulia viongozi hasimu ndani ya chama tawala
cha ZANU-PAFU kwa kupanga kumrithi.
Amesema kuwa yeye anawahudumia watu wa
Zimbabwe na kuwa ataondoka tu ikiwa watu wangetaka
afanye hivyo. Hata hivyo amesema kuwa haondoki na
haendi popote.