Recent Posts

PropellerAds

Thursday, May 12, 2016

Everton yamfuta kazi kocha wake


Klabu ya Everton imempiga kalamu mkufunzi wake Roberto Martinez baada ya kuifunza klabu hiyo kwa miaka mitatu.
Kilabu hiyo ya Martinez ilio katika nafasi ya 12 katika jedwali li ligi ya Uingereza ilishindwa 3-1 na mabingwa wa ligi Leicester siku ya Jumamosi na kupoteza 3-0 dhidi ya Sunderland siku ya Jumatano.
Everton ilipoteza katika nusu fainali ya kombe la FA na lile la Carling msimu huu.
Timu hiyo imeshinda mechi tano pekee nyumbani msimu wote na inatarajiwa kumaliza msimu huu ikiwa na pointi za chini zaidi tangu uzinduzi wa pointi tatu kwa ushindi wowote mnamo mwaka 1981.
Klabu hiyo inatarajiwa kuthibitisha rasmi hatua yao.Kumekuwa na ongezeko la maandamano dhidi ya kocha huyo raia wa Uhispania kutoka kwa mashabiki katika mechi zilizochezwa nyumbani.