Aliyekuwa mgombea wa urais wa tiketi ya chama cha
Republican nchini Marekani, Jeb Bush, amesema kuwa
hatampigia kura Donald Trump katika Uchaguzi wa
Novemba.
Bwana Bush alisema kuwa Trump hana tabia wala
mienendo ya kuwa Rais wa Marekani.
Jeb ni mojawapo wa wanachama mashuhuri wa
Republican kutanganza hadharani kuwa hatompigia
kura Bwana Trump kwa sababu ya kampeni yake ya
kiburi ambayo imegawanya chama cha Republican.
Mnamo Alhamisi Spika wa Bunge, Paul Ryan, alisema
kuwa hatamuunga mkono mfanyabiashara huyo tajiri,
ingawa atakutana naye juma lijalo.
Hata hivyo Bwana Trump ameungwa mkono na
mgombezi wa Urais wa zamani Bob Dole aliyeshindwa
katika uchaguzi na Bill Clinton wa chama cha
Democratic mwaka 1996.
PICHA :Rais Samia alipowasili Uwanja wa Shule ya Msingi Mkata Mashariki
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
alipowasili Uwanja wa Shule ya Msingi Mkata Mashariki kwenye Mkutano wa
hadhara na ...
10 hours ago