Maafisa wawili wa Trafiki wameuawa katika mlipuko wa kujitoa
muhanga wa gari, uliotokea katika makao makuu ya idara ya trafiki mjini
Mogadishu.
Milipuko mikubwa ilisikika katika makao hayo makuu ya Trafiki huko Shangani Mogadishu, na baadaye kufuatia na ufyetuaji risasi.
Wapiganaji wa kundi la al-Shabab wamedai kuhusika.
Katika taarifa yao kundi hilo limedai kwamba shambulio hilo lilipangwa vyema.
Mpiganaji
mmoja aliliendesha gari lililokuwa na vilipuzi na mwingine alijaribu
kuyavamia makao hayo makuu ya trafiki, lakini alipigwa risasi, Abdifatah
Omar Halane, msemaji wa utawala wa mj wa Mogadishu ameliambia AFP.
Mara nyingi Al-Shabab hushambulia maeneo ya jeshi na raia katika kampeni yake ya kuipindua serikali ya Somalia.
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo April 29, 2024
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam April 29,
2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na
za nyuma za Maga...
1 hour ago