Jaji mmoja nchini Honduras ameamua kuwa wanaume wanne wanaweza kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya mwanaharakati wa mazingira, Berta Caceres.
Baadhi ya watu hao ni wanajeshi waliostaafu na wengi bado wanahudumu jeshini. Wengine wameajiriwa na kampuni zinazojenga bwawa kubwa la kuzalisha umeme ambalo ujenzi wake Bi Caceres na vuguvugu la wenyeji limekuwa likipinga.