Recent Posts

PropellerAds

Wednesday, May 18, 2016

Trump: Ninaweza kuzungumza na Kim Jong-un

Marekani
Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump amesema yuko tayari kufanya mazungumzo na kiongozi wa Korea Kaskazini kuhusu mpango wa nyuklia wa taifa hilo.
“Ninaweza nikazungumza naye, Siwezi kuwa na tatizo kuzungumza naye,” Bw Trump alisema kuhusu Kim Jong-un.
Mkutano huo ungekuwa tofauti kabisa na msimamo wa muda mrefu wa Marekani kuhusu Korea Kaskazini.
Hatua hiyo imemfanya mgombea anayeongoza katika kinyang’anyiro cha chama cha Democratic Hillary Clinton kumshutumu Bw Trump na kusema anashangaza kwa kuwaenzi sana viongozi wababe wan chi za nje.
Taarifa iliyotolewa na mmoja wa wasaidizi wa Bi Clinton imesema sera ya mambo ya nje ya Bw Trump usio wa maana yoyote.
Kwingineko, BBC imefahamu kwamba huenda Bw Trump akazuru Uingereza kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Marekani mwezi Novemba.
Wanadiplomasia wanatarajia ziara hiyo ifanyike baada yake kuwa rasmi mgombea urais wa chama cha Republican mwezi Julai.
Mapema wiki hii, Bw Trump alisema dalili zinaonesha huenda asiwe na uhusiano mwema sana na Uingereza.
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na meya mpya wa London Sadiq Khan, ambaye ni Mwislamu, wamemshutumu Bw Trump kutokana na hatua yake ya kupendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani.

Related Posts:

  • Feed my sheep There are many ways to stall out your ministry. You could make a quick list like this one: • Being busy instead of productive• Lack of vision• Low morale• Being scattered more than focused• Trying to please everyone … Read More
  • Trapped in My Own Mind “I can’t live like this anymore!” I cried through sobs. “I just want to die!” I sat on my bed and tried to make sense of what was going on inside. I was tired of the chronic pain, the frequent bouts of illness, and the we… Read More
  • What Do You Feed Your Eyes? What we feed our eyes will eventually rule our hearts. And I’m not just talking about pornography. Jesus says, “The eye is the lamp of the body. So, if your eye is healthy, your whole body will be full of light, but if your… Read More
  • Three Threats to the Joy of This Generation Serious Joy Well now, how shall I come at this? It touches on so many things. In fact, the more I thought about it, the more I thought, “I should write a book on this. I should write a book called Joyful Seriousnes… Read More
  • Is the Joy of the Lord Your Strength? Is the joy of the Lord your strength? This question can be difficult to answer — all of the words are so simple and familiar to Christians, yet the statement can get lost in a fog of ambiguity. When life is simple and swe… Read More