Recent Posts

PropellerAds

Saturday, May 7, 2016

Jiji la London lamchagua Meya Muislamu

Jiji la London limemchagua Meya wa kwanza
Muislamu, Sadiq Khan, aliyekuwa wakati mmoja Waziri
katika chama cha upinzani cha Laba.
Bwana Khan ni mwana wa dereva wa zamani wa bas
jijini London aliyezaliwa Pakistan. Alipata kura milioni
moja na mia tatu elfu.
Hicho ni kiwango kikubwa sana cha kura kuwahi
kupigiwa Meya ye yote jijini London.
Katika hotuba yake ya ushindi, Bwana Khan aliahidi
kuongoza kwa niaba ya wakaazi wote wa London.
Wasimamizi wa kampeni ya mpinzani wake katika
uchaguzi huo Zac Goldsmith, ambaye ni tajiri mkubwa
walishutumiwa kwa kudai kuwa Bwana Khan ana
uhusiano na Waislamu wenye itikadi kali.
Bwana Khan alisema kuwa wakaazi wa London
wamepiga kura ya umoja na kuponza mgawanyiko.
Ushindi huo ni wa kumtia moyo kiongozi wa chama cha
Labour Jeremy Corbyn.
Chama chake kilipata ushindi dhaifu katika maeneo
mengine ya nchi katika uchaguzi huo.

Related Posts:

  • Ruto asubiri uamuzi muhimu ICCMakamu wa Rais wa Kenya William Ruto atafahamu leo iwapo kesi inayomkabili katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) itatupiliwa mbali. Mwanahabari Joshua arap Sang, aliyeshtakiwa pamoja na Bw Ruto, pia atafahamu leo iwap… Read More
  • MAGAZETI YA TZ LEO,APRIL 7 Read More
  • Ted Cruz amshinda Trump mchujo WisconsinMgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Ted Cruz ameshinda mchujo wa chama hicho katika jimbo la Wisconsin, hilo likiwa pigo kubwa kwa Donald Trump. Katika chama cha Democratic, Bernie Sanders alipata ushindi mk… Read More
  • FELEX NTEBENDA:MARUFUKU VIROBAMkuu wa Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda amepiga marufuku uuzwaji wa kilevi aina ya kiroba katika mkoa huo. Alisema uamuzi huo unatokana na vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa kushindwa kufanya kazi na kulewa wakati wa kazi. Ai… Read More
  • Hatimaye Magufuli atoka nje ya nchiDar es Salaam. Rais John Magufuli leo anakwenda Rwanda, ikiwa ndiyo ziara yake ya kwanza ya nje ya nchi tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo, Novemba 5, mwaka jana. Rais Magufuli alisimamisha safari za nje kwa watumishi wa … Read More