Recent Posts

PropellerAds

Monday, May 9, 2016

Jaji adai ubakaji ni kawaida kwa wanaume Waafrika



Jansen
Jaji mmoja mzungu nchini Afrika Kusini ameshutumiwa vikali baada ya kudaiwa kusema kwenye mitandao ya kijamii kwamba ubakaji ni kawaida kwa wanaume weusi.
Jaji Mabel Jansen alisema unajisi wa watoto na wasichana na pia ubakaji wa wanawake ni jambo la “kufurahiwa” la kupitisha wakati miongoni mwa Waafrika.
Kadhalika, amenukuliwa pia akisema hajawahi kukutana na msichana mweusi ambaye hajawahi kubakwa.
Kampeni imeanzishwa ya kutaka afutwe kazi.
Akijitetea, jaji huyo amesema amefasiriwa vibaya na kwamba matamshi hayo yametumiwa vibaya nje ya muktadha.
Jaji Jansen anadaiwa kutoa matamshi hayo kwenye mawasiliano na mwanaharakati Gillian Schutte kwenye Facebook mwaka jana lakini yamesambazwa sana wikendi.
"Katika utamaduni wao, mwanamke yuko hapo kuwaburudisha. Mwisho. Hutazamwa kama haki yao na mtu hatakiwi kuomba ruhusa kutoka kwa mwanamke,” jaji huyo amenukuliwa akisema.
Wakili mashuhuri Afrika Kusini Vuyani Ngalwana amesema matamshi hayo ya jaji huyo yanawaharibia sifa wanaume wote weusi na kuwaonesha kama wabakaji.
Amesema ni ya kushangaza sana, kwa mujibu wa gazeti la Business Day.
Bw Ngalwana amesema Tume ya Huduma za Mahakama inafaa kumtaka afafanue matamshi hayo kabla ya kumchukulia hatua.
Msemaji wa chama tawala cha African National Congress (ANC) amesema anashuku kuna majaji wengi wenye mtazamo wa kibaguzi.
Utawala wa Wazungu ambao ulihalalisha ubaguzi wa rangi ulifikia kikomo nchini Afrika Kusini mwaka 1994.

Related Posts:

  • Whatever Is Not from Faith Is Sin — Really? People from the time of John Chrysostom (347–407) have tried to limit the meaning of Paul’s words in Romans 14:23, “Whatever does not proceed from faith is sin.” Chrysostom cautions, “Now all these things have been sp… Read More
  • Most-Used Promises Let me answer this in three stages that more or less correspond to three stages of my life, although they really do overlap. They overlap but they have different starting places. My memory of my childhood isn’t good enoug… Read More
  • All Things Were Created Through Him and for Him God’s Sovereignty over Sin First, on a porch in Asheville, North Carolina, I was reading during the last half of July the Old Testament book of 2 Chronicles. As in every year when I get to this portion of Scripture, I a… Read More
  • If I Were 22 Again “What would you do if you were 22 again?” I was recently asked that question as part of a conference on world missions. I turned 22 in the middle of my senior year at Wheaton College. I was an English Literature major and h… Read More
  • Real Marriage Real Marriage One, it is not a wedding, because it is not a marriage. Therefore, attending it as a wedding is to be false like everyone there is being false. There is no such thing as a so-called same-sex marriage. God … Read More