Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, May 17, 2016

Matapeli wa You Tube wafungwa jela


Wanachama wanne wa kundi lenye utata la Trollstation katika mtandao wa Youtube wamefungwa jela kutokana na wizi wa mabavu na utekaji nyara bandia.
Kundi hilo lilihusishwa katika wizi wa mabavu wa bandia katika eneo la kumbukumbu za uchoraji mjini London pamoja na utekaji nyara bandia katika eneo la Tate nchini Uingereza mnamo mwezi Julai 2015.
Idhaa hiyo ilio na wateja 718,000 imejijengea sifa kwa kutengeza video bandia mjini humo.
Mwanachama wa tano alifungwa mnamo mwezi Machi kufuatia utapeli wa tukio la bomu.
''Utapeli huo huenda waliouona kama wa kawaida,bila kujua kwamba ulikuwa unawapa dhiki raia wa kawaida ambao wanafaa kuendelea na bishara zao bila kuogofywa''.
''Tunatumai kwamba kifungo hicho kitakuwa mfano kwa wale wanaotekeleza vitendo vya utapeli kama hivi ambavyo haviwezi kukubalika kuendelea mjini London'',alisema Robert Short,afisa wa mashtaka katika huduma ya Crown Prosecution Service.