Recent Posts

PropellerAds

Friday, May 13, 2016

Brazil yapata kiongozi mpya

Temer
Kaimu rais mpya wa Brazil, Michel Temer, ametoa wito kwa raia wa taifa hilo kuunga mkono serikali yake na kufanya kazi kwa pamoja kujenga upya sifa ya serikali baada ya mgogoro wa kisiasa ulioikumba nchi hiyo.
Bw Temer amesema michezo ya Olimpiki mjini Rio mwezi Agosti, itatoa fursa kwa Brazil kuuonyesha ulimwengu hali halisi ya kiuchumi na kisiasa nchini humo.
Alikuwa akizungumza katika hotuba yake ya kwanza kabisa tangu kuchukua hatamu kutoka kwa Dilma Rousseff aliyeondolewa madarakani kwa muda akisubiri mchakato wa kumtimua ukamilike.