Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, May 10, 2016

Waziri amtaka Gardner kuomba radhi Kwa lady Jay dee

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto, Hamis Kigwangalla, amemtaka
mtangazaji wa Clouds FM, Gardner G Habash
kumuomba radhi aliyekuwa mke wake, Lady Jaydee
kwa ‘kile alichokiita’ kama udhalilishaji kwake na kwa
wanawake wote.
Wikiendi iliyoisha imesambaa video mtandaoni
ikimuonesha mtangazaji huyo akiongea kwenye
tamasha alilokuwa mshereheshaji: My name is Captain
Gardner G Habash all the way from Clouds FM, Jahazi
hatari sana. Na sina neno na yule mtoto wa kike.
Nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi.”
Video hiyo imesababisha hasira kubwa kwa mashabiki
wa Jaydee na watu wengi kwa ujumla.
“Ndg. Gardner amefanya udhalilishaji mkubwa si tu
Kwa @JideJaydee bali ametukana wanawake wote.
Mimi #BaloziWaWanawake namtaka aombe radhi,”
ameandika mheshimiwa Kigwangalla kwenye Twitter.
“Natoa rai kwa uongozi wa @cloudsfm kumtaka Ndg.
Gardner afute kauli yake na aombe radhi kwa
@JideJaydee na kwa umma ili kulinda heshima yao,”
ameongeza.
“Jamani, sijui ugomvi wao wala sina interest ya kujua,
sema alichokisema G na nikasikia ni katika
tusiyosemaga hadharani kwa heshima ya mama,”
amefafanua.
“Sina maana wamchukulie hatua. Watambue tu kosa
lake na wamtake kwa heshima kwa mama aombe
radhi. Mimi ni mtumishi namba 2 kwenye Wizara
inayosimamia ‘mambo ya wanawake’! I know what I
am talking about hapa.”

Related Posts:

  • Mbona bado kuna njaa duniani? Umoja wa Mataifa umetangaza njaa sehemu kadha nchini Sudan Kusini, ambayo ni ya kwanza kutangazwa popote pale duniani katika kipindi cha miaka sita. Pia kuna onyo la kutokea njaa kaskazini mashariki mwa Nigeia, Somalia … Read More
  • Tanzania kuimarisha biashara na Uganda Serikali ya Tanzania imesema kuwa itaimarisha biashara yake na Uganda kwa lengo la kuinua uchumi wa raia wa mataifa hayo mawili. Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa tayari Tanzania imeanza kutekeleza miradi … Read More
  • Tumbili 57 wauawa kwa sababu ya ubaguzi Japan Hifadhi moja wa wanyama ambayo ni ya kuwahifadhi tumbili wa barafu imewaua tumbili 57, ambao ilikuwa ikiwahifadhi baada ya kugundua kuwa nyani hao walikuwa na maumbile ya kijenetiki ya familia tofauti . Hifadhi hiyo ya T… Read More
  • Mkuu wa majeshi afutwa kazi Gambia Rais wa Gambia Adama Barrow amemfuta kazi mkuu wa majeshi Jenerali Ousman Badjie. Jenerali Badjie alitangaza utiifu wake kwa rais aliyeondoka madarakani Yahya Jammeh baada ya uchaguzi w… Read More
  • Wabunge waidhinisha kilimo cha bangi Uholanzi Bunge la chini nchini Uholanzi limeidhinisha kuhalalishwa kwa kilimo cha bangi. Mswada huo ulioidhinishwa, utawakinga wakulima wa bangi ambao wanatimiza masharti fulani dhidi ya kuadhibiwa. Mswada huo bado haujaidhinishwa k… Read More