Recent Posts

PropellerAds

Saturday, May 28, 2016

Trump apata wajumbe wa kutosha Marekani


Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Donald Trump amefikisha idadi ya wajumbe ya kupata uteuzi wa chama hicho kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Bw Trump ambaye aliwashinda wagombea wengine 16 wa chama hicho ameripotiwa kupata wajumbe 1,238 mmoja zaidi ya inavyohotajika.
Chama cha Republican kinataraijiwa kukamilisha uteuzi wao katika mkutano wa chama hicho utakaofanyika huko Cleveland mnamo mwezi Julai.
Iwapo atathibitishwa ,bw Trump atakabiliana na aliyekuwa waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Hillary Clinton au seneta wa Vermont Bernie Sanders ambao wanashindania uteuzi wa chama cha Demokrat.
Siku ya Jumatano,bilionea huyo wa New York alipanga kufanya mjadala na Bernie Sanders katika runinga mjini California kabla ya uchaguzi wa mchujo wa tarehe 7 mwezi Juni.
Bw Sanders alikubali kushiriki katika mjadala huo katika ujumbe wake wa Twitter uliosema: ''Game on''.