Mwanamume anayetarajia kuwa mgombea mkuu wa upinzani kwa urais
katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, anatarajiwa kufika mbele ya
mahakama leo kujibu mashtaka yanayaomkabili ya kuwaajiri mamluki kutoka
mataifa ya nje.
Mawakili wa Moise Katumbi wanasema Gavana
huyo wa zamani wa jimbo lililo na utajiri wa madini - Katanga,
alikabidhiwa barua ya kufika mahakamani mwishoni mwa juma na anatakiwa
kufika mbele ya mwendesha mashtaka nchini humo siku ya Jumatatu.
Nyumba yake ilisakwa na walinzi wa serikali siku ya Jumamosi.
Katumbi amekana mashtaka na ameishutumu serikali kwa kutumia njia za kumchafulia jina.
Ubalozi wa Marekani mjini Kinshasa pia umetilia shaka tuhuma hizo.
Rais
Joseph Kabila ambaye yupo madarakani tangu mwaka 2001 bado hajabainisha
iwapo atajiuzulu mwaka huu kama inavyo takiwa kwenye katiba ya nchi
Barrick Tanzania yatoa elimu ya usalama kazini na utunzaji wa Mazingira
-
Elimu ya afya na usalama mahali pa kazi inaendelea kuwafikia wananchi
mbalimbali ambao wanatembelea banda la maonesho ya kampuni ya dhahabu ya
Barrick ku...
2 days ago