Recent Posts

PropellerAds

Saturday, May 21, 2016

Magufuli amfuta kazi waziri kwa kuwa mlevi


Waziri wa mambo ya ndani nchini Tanzania Charles Kitwanga amefutwakazi kutokana na sababu ya kuwa mlevi akiwa kazini.
Kwenye taarifa, rais John Magufuli alisema kuwa bwana Kitwanga alienda bungeni na kujibu swali la mbunge akiwa mlevi.
Hata hivyo bwana Kitwanga hajasema lolote.

Rais Magufuli ambaye aliingia ofisini mwaka uliopita aliahidi kupambana na ufisadi na awewafuta kazi maafisa kadha kuhusiana na suala la ufisadi.
Lakini waandishi wa habari wanasema kuwa kufutwa kwa bwana Kitwanga ni jambo la kushangaza kwa sababu amekuwa rafiki wa rais kwa siku nyingi