Recent Posts

PropellerAds

Friday, May 6, 2016

Mfanyabiashara Jacob Juma auawa Nairobi


Juma

Mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma, ambaye amekuwa akizua mjadala mitandaoni Kenya kutokana na ujumbe wake anaoandika hasa kwenye Twitter, ameuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi.
Taarifa zinasema Bw Juma alipigwa risasi na watu ambao walikuwa wakiendesha pikipiki alipokuwa akielekea nyumbani kwake mtaa wa Karen mwendo wa saa nne usiku.
Gari lake lilipatikana na zaidi ya matundu 10 ya risasi.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la Kenya, polisi wanasema hakuna kilichoibiwa kutoka kwenye gari lake. Simu zake mbili na pesa vilipatikana ndani ya gari.
Bw Juma alikuwa mwanakandarasi ambaye pia alihusika katika sekta ya uchimbaji madini.

 
Alikuwa mkurugenzi katika kampuni ya Erad iliyoshtaki Bodi ya Taifa la Nafaka na Mazao kuhusu kandarasi. Alitaka alipwe jumla ya Sh500m na bodi hiyo.
Agosti mwaka jana, alimshtaki Gavana wa jiji la Nairobi Dkt Evans Kidero akitaka akaunti zake za benki zifungiwe kwa tuhuma kwamba gavana huyo alihusika katika ufujaji pesa kampuni ya sukari ya Mumias Sugar.
Bw Juma pia alimshtaki waziri wa madini Najib Balala mwaka jana baada ya leseni ya kampuni yake ya madini ya Cortec Mining kupokonywa leseni.
Miaka 10 iliyopita, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, Bw Juma pia alimshtaki bintiye rais wa zamani Daniel arap Moi kuhusiana na shamba la ekari 250.
Aidha, aliwasilisha kesi mbili dhidi ya Naibu Rais William Ruto.
Amekuwa akikosoa sana serikali ya Rais Uhuru Kenyatta na ni mmoja wa waliokuwa wakiishinikiza sana kuhusiana na sakata ya Eurobond.

Related Posts:

  • What Is the Gospel? A Message from God What exactly do Christians mean when they talk about the “gospel of Jesus Christ”? Since the word “gospel” means “good news,” when Christians talk about the gospel, they’re simply telling the good news ab… Read More
  • Reach Your Destiny with The Words You Speak If you want to reach your destiny and I can assume you want to, because you came to the title of this article, you have to learn to watch what you speak if you are serious enough. Your words can create your destiny… Read More
  • "Your Destiny Is Within Your Reach!" Scripture: Phillipians 3:12-14 Title: “Your Destiny Is Within Your Reach!” I. Introduction: The one thing that really keeps us from obtaining our destiny and from going to the next level in God and that holds us back is o… Read More
  • Women in Society: The Challenge and the Call A Surprising Phone Call I was working as an unsalaried assistant in my husband’s senate office when, one day in 1982, I was surprised to receive a call from the White House. President Reagan wanted to know if I would acce… Read More
  • Know What Not to Say Christians should be the most careful speakers in the world. We ought to be characterized by two kinds of trembling when it comes to words: we should tremble at the words God speaks and we should tremble at the words we spea… Read More