Recent Posts

PropellerAds

Thursday, May 12, 2016

Walimu walipwa vifaranga badala ya mshahara Uzbekistan


Mji mmoja nchini Uzbekistan umekua ukiwapa waalimu wake kuku kama mshahara badala ya pesa. Mamlaka za mji wa Nukus katika jimbo linalojitawala la Karakalpakstan wamekua wakitia vifaranga wachanga kwa walimu kutokana na uhaba wa pesa nchini humo.
Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Marekani{Radio Ozodlik} kimemnukuu mwalimu mmoja akilaani hatua hiyo kama aibu kubwa kwa mamlaka.
Mwalimu huyo aliyeghadhabishwa na hatua hiyo amesema hataki vifaranga kwa sababu anaweza kuwapata sokoni, lakini wanataka pesa zao.
Vifaranga wanaotolewa kama mshahara wana gharama ya dola mbili kila mmoja, ikiwa ni maradufu bei inayouzwa vifaranga sokoni.
Mamlaka za Uzbekistan hazikubalii uhuru wa vyombo vya habari na raia wa huko hutegemea vyombo vya habari vya kimataifa kutoa sauti yao, ila hawajitambulishi.
Uzbekistan imekumbwa na uhaba wa fedha kwa miaka sasa hali inayosababisha serikali kuchelewesha mishahara ya wafanyikazi na malipo ya uzeeni.
Mapema mwezi huu wafanyikazi wa serikali katika mji mkuu,Tashkent walilalamikia kwamba hawakuwa wamelipwa mshahara kwa miezi miwili kwa sababu benki hazikuwa na pesa.

Related Posts:

  • bandari ya Dar es salam kupanuliwa kwa gharama ya $ 305.Tanzania inasema kuwa itapokea dola milioni 305 kama mkopo kutoka kwa Benki ya Dunia, kugharamia upanuzi wa bandari kwenye mji wa Dar es Salaam. Bandari hiyo ndiyo inaunganisha mataifa ya Afrika ambayo hayapakani na bahari ya… Read More
  • 7 Tips for Network Marketing Successmarketing (also known as direct sales or multilevel marketing) is all about-- housewives buying and selling Tupperware while gossiping and eating finger sandwiches, or a high-pressure salesperson trying to convince you how ea… Read More
  • Ajiuzulu baada ya papa kumtaka asambaze kondomuKiongozi wa kanisa katoliki anayewasaidia raia wa Malta amejiuzulu kufuatia mgogoro na Vatican kuhusu mpango wa kusambaza mipira ya kondomu kulingana na kanisa hilo. Mathew Festing mwenye umri wa miaka 67 alijiuzulu baada ya … Read More
  • JE? NI KICHWA GANI UNACHOTUMIA KUFANYA MAAMUZI..? Na Mwl John C Ntogwisangu_ Mwanaume ana Vichwa viwili, Kimoja kipo juu na kingine kipo chini. Vichwa Vyote vina Kazi yake na umuhimu wake Katika Mwili, hakuna kilicho bora kuliko kingine. Vichwa hivi mara nyingi hupingana … Read More
  • Al-Shabab washambulia hoteli Mogadishu Wanamgambo wanaoshukiwa kuwawanachama wa al-Shabab wameshambuliahoteli moja katika mji mkuu wa SomaliaMogadishu.Watu hao wenye silaha wameingia kwenyehoteli hiyo baada ya kulipuliwa kwa mabomumawili kwenye lango la kuingia k… Read More