Bw Valls alikuwa akiongea kwenye mkutano wa pamoja wa waandishi wa habari mjini Canberra nchini Australia na mwenzake waziri mkuu Malcolm Turnbull.
Wiki iliyopita DCNS iliwabiku washindani kutoka Japan na Ujerumani na kushinda kandarasi hiyo ya gharama ya dola billioni 39 ya kujenga manowari 12 kwa Australia.
Kampuni hiyo inasema kuwa chombo hicho chenye uzito wa tani 4500 ndicho hatari zaidi kuwai kujengwa.