Recent Posts

PropellerAds

Tuesday, May 3, 2016

IMF: Uchumi wa Tanzania waongoza Afrika Mashariki

Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu zaidi cha ukuaji wa uchumi wake mwaka huu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la fedha la kimataifa - IMF.
Katika ripoti yake iliyotolewa hii leo Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Kasi hiyo ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni ya pili tu nyuma ya Ivory Coast baina ya mataifa ya Kusini mwa jangwa la Sahara .Ivory Coast inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 8.5%.
Katika kanda ya Afrika Mashariki ,uchumi wa Kenya ndio wa pili kwa kasi ya ukuaji kwa asilimia 6%.
IMF hata hivyo inasema kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua kwa mwaka wa pili mfululizo kutokana na kudorora kwa viwango vya uzalishaji na hivyo uwekezaji.
Kwa mujibu wa shirika la fedha la kimataifa - IMF, eneo hilo linakadiria kushuka kwa ukuwaji wa uchumi kwa asilimia 3 mwaka huu.
Kiwango hicho ni cha chini kabisa kuwahi kushuhudiwa katika miaka 15
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Aidha Zambia pia imeathirika vibaya kutokana na ukosefu wa soko la kimataifa la shaba yake.
Ripoti hiyo inaitaja Afrika Kusini kama moja ya mataifa ambayo kiwango chake cha ukuaji kimedorora kwa kiasi kikubwa mno.
Katika orodha ya mataifa yanayotarajiwa kuwa na kiwango cha juu cha ukuaji Kusini mwa jangwa la sahara Ivory Coast ndio inayoongoza.
Orodha ya mataifa ya kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara na viwango vya kasi ya ukuaji wa uchumi 2016.
  1. Ivory Coast 8.5%
  2. Tanzania 6.9%
  3. Senegal 6.6%
  4. Kenya 6%
  5. Zambia 3.4%
  6. Nigeria 2.3%
  7. Afrika Kusini 0.6%

Related Posts:

  • The Deep Riches and Wisdom and Knowledge of God One of the highest points in my short, six-year teaching career in the Biblical Studies department at Bethel College was in the spring of 1977. I had spent the entire semester on Romans 9–11 leading about a dozen adva… Read More
  • On My Wedding Day The wedding day has finally come. Tomorrow, Lord willing, I will no longer be not-yet-married. In a month or year or five years, people will ask us how marriage is going. We didn’t want to have to settle for how we feel i… Read More
  • Choosing the Path of Holiness Asking Christ into our lives is the single most important thing we can ever do. But what happens after that? Does it matter how we live our lives if we already have the assurance that we will be with Christ in heaven when we… Read More
  • Ask God to Forgive You, Not Excuse You God exists everywhere and everywhen. He is eternal and omnipresent. And not only is he present everywhere, he is everywhere pursuing us. He is the hunter, the king, the husband, approaching us at an infinite speed. Central… Read More
  • Children Need a Crisis of Faith  My wife and I have five children. Our oldest two have exited childhood and are adventuring into the uncharted territory of their young adulthood. Our younger three are navigating the tricky waters of adolescence. A… Read More