Recent Posts

PropellerAds

Monday, May 2, 2016

Maelfu wamuaga Papa Wemba Kinshasa

Papa Wemba
Maelfu ya waombolezaji walijitokeza kuadhimisha misa ya wafu kwa heshima ya mwanamuziki nyota wa muziki wa Soukus na Rhumba raia wa Jamhuri ya Congo Papa Wemba.
Waomboloezaji walipiga foleni ilikupata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kwa msanii huyo nguli aliyeaga dunia juma lililopita alipokuwa akiwatumbuiza mashabiki wake huko Abidjan Ivory Coast.
Mwili wake umewekwa katika majengo ya bunge mjini Kinshasa.
Serikali imetangaza siku tatu za maombolezi kuanzia leo hadi jumatano atakapozikwa.

Msanii huyo nguli alikonga nyoyo za wapenzi wa muziki wa Soukus nchini DRC na kote duniani kwa kipaji chake cha kipekee na sauti isiyokuwa na mfano.
Wengi waliitambua sauti hiyo ya na utunzi wake.
Alikuwa ni mtumbuizaji kamili.
Gwiji huyo wa muziki wa Lingala alizaliwa mnamo Juni 14 mwaka 1949, katika eneo la Lubefu - Wilaya ya Sankuru nchini Congo.
Jina lake halisi ni Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba.
Yeye alianza kazi ya muziki akiwa na umri mdogo mno.
Alikuwa akimfuata mamake katika matanga na hivyo akaibukia kuwa mtunzi wa nyimbo za kuomboleza.
Mfalme huyo wa muziki wa Rhumba, mwenye umri wa miaka 66 aliaga dunia ghafla 24 April akiwa nchini Ivory Coast .

Related Posts:

  • Nine Words for Every Marriage Someday my children will introduce me to the person they intend to marry. When they do, there are three sentences — nine simple words total — that I want to know they can say, in earnest, before they can have my blessing:&… Read More
  • FAIDA ZA UFUGAJI NYUKI FAIDA ZA UFUGAJI NYUKI : Watu wengi duniani hudhania kwamba faida ya nyuki ni uzalishaji wa asali tu, na si vinginevyo. Lakini karne za hivi karibuni jinsi binaadamu walivyoanza kujihusisha na tafiti za wadudu mbalimbali, wa… Read More
  • certain requirements we must fulfill before God will listen to our prayers. We Must Belong to God. “There is one God and one mediator between God and man, the man Christ Jesus” (1Timothy 2:5). Because Jesus is the mediator between us and God, we must give Him our total allegiance. Before I yield… Read More
  • What About Those Who Have Never Heard? Dear _____, You asked what happens to people who live far away from the gospel and have never heard about Jesus and die without faith in him. Here is what I think the Bible teaches. God always punishes people because of … Read More
  • The Best Church Leader Is a Team Plurality. It’s a weighty word that reminds us that ideas have consequences. By plurality, I’m talking about shared leadership. It’s a way of referencing the consequential idea that leadership in the New Testament was a te… Read More