Bw Kasich alitoa tangazo hilo kwenye mkutano na waandishi wa habari nyumbani kwake katika jimbo la Ohio.
Hatua hiyo inatoa fursa kubwa kwa Bw Trump kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwezi Novemba.
Trump anasema kuwa ana matumaini ya kuchangisha zaidi ya dola billioni moja kwa kampeni yake.