Ni zaidi ya miaka 20 sasa tangu taifa hilo lijipatie uhuru wake na inaonyesha kuwa hatua hiyo haijasahaulika.
Watu hukasirishwa kwa kile wanasema ni hali ya kujikokota kwa serikali kuwapatia huduma kama vile nyumba,umeme na maji na hivyobasi kuamua kufanya uharibifu.
Lakini visa hivyo vimekosolewa na serikali kwa kuwa waandamanaji uharibu vitu muhimu kama vile shule,maktaba na kliniki.
Mwishowe jamii hizo husalia zikihitaji huduma hizo,serikali inasema.